Description
Sebastiani mfiadini (alifariki miaka ya 288 hivi) alikuwa Mkristo aliyeuawa wakati wa dhuluma ya kaisari Diocletian dhidi ya imani hiyo.
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini. Wa kwanza wanaadhimisha sikukuu yake tarehe 20 Januari, wa pili tarehe 18 Desemba.